HABARI WATANZANIA.
Ningependa kuleta mada hii mezani kwenu ili tuweze kuijadili.
kumekuwa na malalamiko mengi kuhusu ndoa au uchumba kuvunjika mapema, je unadhani ni sbabu zipi changizi na nini kifanyike.
kwa upande wangu nimejaribu kuchunguza na kuona kuwa sisi(wanaume) si wakweli; hivyo tumewafanya wanawake waishi bila kutuamini.
kutokana na mtazamo huo wamejikuta wakifanya kama ambavyo tunafanya sisi ili kujaribu kuturudisha katika tafakuri.
na kwakuwa wanaume hatupendi kusalitiwa bali kusaliti tumejikuta kuwa walalamikaji na kuvunja uhusiano huku tukisahau kuwa hata sisi ni wasaliti.
Tujaribu kuwa wakweli pale tunapowatongoza mabinti ili waingie katika uhusiano wanaoufahamu.
NANI ALAUMIWE? JADILI UNAVYOELEWA